SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatano, 15 Machi 2017

T media news

Kutana na Mtanzania pekee anaewania uongozi ndani ya FIFA


Rais wa zamani wa TFF Leodgar Tenga ambaye kwa sasa ni mjumbe wa kamati ya utendaji ya CAF, anagombea nafasi ya kuingia kwenye baraza kuu la FIFA.
Gianni Infantino baada ya kuingia madarakani, aliongeza wigo wa wajumbe wa baraza kuu la FIFA, mwanzoni lilikuwa na wajumbe 24lakini ameongeza hadi kufikia wajumbe 36.
Kwa hiyo Afrika na yenyewe imeongezewa idadi ya wajumbe wa kuingia kwenye baraza kuu la FIFA, nafasi hizo za wajumbe wa baraza kuu kwa upande wa Afrika zimegawanywa kwa zones. Kuna mwakilishi kutoka nchi zinazozungumza lugha ya Kifaransa (Francophone  countries) sambamba na mwakilishi kutoka nchi zile zinazozungumza English (Anglophone countries).
Tenga (Tanzania) na Kwesi Nyantakyi (Ghana) ambaye ni rais wa chama cha soka cha nchi hiyo ndio wanagombea nafasi moja, kesho watakuwa wanapigiwa kura ili kumpata mjumbe mmoja atakaeingia kwenye baraza kuu la wajumbe wa FIFA.
Iwapo  Tenga atafanikiwa kupigiwa kura nyingi, ataingia kwenye baraza kuu la FIFA na itakuwa ni faida kwa Tanzania.
Wajumbe hao watakaochaguliwa, wataungana na wajumbe wengine kukamilisha idadi ya wajumbe 36 wa baraza kuu la FIFA ambapo watakutana kwa mara ya kwanza kati ya October 13 na 14 huko Zurich, Uswis.