ambao wanayahofia maisha yao endapo watarudi nchini Iran
Trump amempongeza Albanese kwa kitendo hicho cha kiungwana cha kuwa hifadhi wachezaji hao ambao wengine wanataka kurudi nchini Iran wakidai kuwa endapo wasiporudi serikali ya Iran itaziumiza familia zao
Siku ya tarehe 2 mwezi huu baadhi ya wachezaji wa timu ya Taifa ya wanawake ya Iran waligoma kuimba wimbo wa Taifa lao wakati wa ufunguzi wa mechi ya mpira wa miguu kati ya timu ya Taifa ya Iran na Korea kusini mechi ya mashindano ya Asia women's Cup
Wachezaji hao waligoma kuimba wimbo huo ikiwa ni ishara yao ya kuipinga serikali ya Iran ambayo wakati huo tayari ilikuwa imeshaingia vitani na Marekani na Israel
Baada ya mechi hio ambayo timu hio ya Iran ilifungwa bao 3-0 hao walikataa kurudi nchini Iran wakidai kuwa serikali ya Iran imewaona kama wasaliti na hivyo maisha yao yapo hatarini, huku baadhi wakidai kuwa familia zao zilizopo nchini Iran zinatishiwa maisha endapo wao hawatorejea
Wachezaji 5 wa timu hio walitoroka kambi na kukimbilia kwenye mamlaka za Australia kwaajili ya usalama wao ambapo kwasasa wanalindwa na vyombo vya usalama vya Australia , wachezaji wengine bado wapo nchini humo nao wakiwa chini ya ulinzi kuepuka kufanyiwa chochote

