SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumanne, 12 Septemba 2017

T media news

Ifahamu Simu ya Kwanza ya Mkononi Duniani iliyoingizwa Sokoni Mwaka 1983 na Kuuzwa Mil 8

Zaidi ya miaka 42 iliyopita simu ya kwanza ilipigwa kutumia simu ya mkononi, simu hiyo ya kwanza ya mkononi ilitengenezwa na kampuni ya Motorola. Ilikuwa mwezi wa 4 tarehe 3 mwaka 1973 walijaribu kupiga simu kwa kutumia simu hiyo ya kwanza ya mkononi iliyokuwa inafahamika kwa jina la Motorola DynaTAC.

Mfanyakazi wa Motorola aitwaye Marty Cooper alitumia simu ya mkononi kupiga simu kwenda ofisi yao (kwenye simu ya mezani), ilipoita na kupokelewa alisema, “Napiga simu kutaka kufahamu kama nasikika vizuri upande huo.”

Simu hii ilikuja kuingia sokoni mwaka 1983 baada ya muda kidogo ikitumia jina la Motorola DynaTAC 8000x na hii ndiyo simu ya kwanza ya mkononi kuingia sokoni na watu kuweza kununua. Na ilikuwa inauzika kwa bei ya juu sana, dola 3995 za kimarekani za wakati huo, ambayo ni si chini ya Tsh 8,000,000 za kitanzania.