SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 4 Novemba 2016

T media news

Shabiki wa Man United: Fukuza Mourinho au niue mbwa wangu


Mtandao wa jana ulilipuka kwa post nzito baada ya Manchester United kupoteza mchezo mwingine tena chini ya utawala wa Jose Mourinho.

Mashetani Wekundu hao wamefungwa mabao 2-1 dhidi ya Fenerbahce kwenye Michuano ya Europa, na kuweka rehani mataumaini yao ya kufuzu hatua ya mtoano.

Na kufuatia kipigo hicho ambacho ni cha tano kwenye michuano yote msimu huu, baadhi ya mashabiki waliamua kumalizia hasira zao kwenye mitandao ya kijamii na kutaka Mourinho afukuzwe na arejeshwe Sir Alex Ferguson, ambaye alistaafu mwaka 2013.