SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 6 Novemba 2016

T media news

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 85 & 86 (Riwaya inawafaa kuanzia miaka 18 na kuendelea )


MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

ILIPOISHIA

Baada ya dakika moja, simu akakabidhiwa Phidaya

"Eddy usitoe chochote"

Sauti ya Phidaya ilisikika, ikiambatana na mlio wa risasi kisha simu ikakatwa, nikajaribu kupiga tena huku mwili mzima ukinitetemeka ila haikupatikana tena, na saa yangu ya mkononi ikinionyesha yamesalia masaa kumi na tano tu.

ENDELEA

Nikabaki nikiwa nimeizhik simu yangu nisijue nini cha kufanya. Nikapata wazo la kumpigia mmoja wa waongozaji wa tangazo la magari ya Ford, ambaye alitokea kuwa rafiki yangu sana

"Smith, mimi Eddy"

"Vipi kaka, mbona unahema sana?"

"Nahitaji msaada wako"

"Upo wapi?"

"Nipo Dar es Salaam, umesha rudi Marekani?"

"Hapana, bado nipo Dar, labda kesho kutwa naweza kuondoka kuna vipande vya lile tangazo, vinamapungufu, tumeamua kuvitengeneza upya"

"Ahaa mupo wapi?"

Smith akanielekeza walipo, nikakodi tena pikipiki hadi walipo kwenye moja ya godauni, ambapo wamepafanya kama studio, wakitumia 'blue screen' wakitengeneza mazingira kama ya Arusha.

"Vipi Eddy mbona kama una wasiwasi?"

"Kaka nina matatizo makubwa sana"

Nikanza kumuadisia Smith, tukio moja baada ya jengine, sikumficha kitu cha aina yoyote.

"Eddy nakuahidi hakuna kitakacho haribika, nitakusaidia kaka yangu"

"Pesa yote hiyo utaitoa wapi Smith, wakati bado upo Tanzania?"

"Njoo uone"

Tukaingia ña Smith kwenye moja ya chumba, ambapo tukakuta Mtu anaye fanana na mimi kila kitu.

"Huyu nane ni nani?"

"Tumemtafuta mtu wa kufanana na wewe, ili aweze kurekebisha baadhi ya vipande, tulijaribu kukupigia simu ila hatukukupata"

Hapa ndipo nilipo amini duniani watu ni wawili wawili, Jamaa hadi kuzungumza anafanana na mimi.

"Umaitwa nani?"

"Fred"

"Duuu jamaa anafanana na mimi"

Nilizungumza huku nikiwa ninacheka kwani sikuamini kukutana na mtu anaye fanana na mimi, kwa asilimia zaidi ya tisini.

"Eddy huyu umnaonaje kakakusaidia katika swala zima la wewe kuoa"

"Apo Smith umenena jambo la maana"

"Alafu una bahati kwa maana ndio amemaliza kushooti vipande tulivyo vikosea"

Nikaanza kumuelezea fredy historia yangu yote kuanzia mwanzo hadi mwisho, nikamuelezea mazingira yate ya nyumbani, pamoja na mtafaruku uliopo kati yangu na mama

"Nimekuelewa Eddy, ila huoni kwamba itakua hatati siku wakigundua kwamba mimi sio wewe?"

"Hawawezi kugundua, kikubwa ni weww kuwa karibu sana na mimi, kila jambo ambalo utaona linakutatiza nijulishe kwa njia ya meseji"

"Ila kuna kitu kingine ambacho ni kigumu"

"Kitu gani?"

"Na mimi nina mke, ila bado sijamuoa"

"Ahaaaa Fredy, hii ni ishu kati yangu mimi na wewe, pia nitakupa kiasi chochote cha pesa"

"Utachukua muda gani kurudi, kutoka kuko Somalia?"

"Haitazidi mwezi mmoja"

"Ahaa kaka, huoni nitampoteza mke wangu"

"Mkeo anaishi wapi?"

"Mbagala rangi tatu"

"Ndipo ulipo kua ukiishi wewe?"

"Ndio ninapo ishi"

"Fanya hivi, mimi ninakupeleka nyumbani kwetu, mimi nielekeze kwako, nitazungumza na mkeo"

Fredy akajifikiria kwa dakika kadhaa, akakakubali kuufanya mchezo wa hatari, uliopo mbele yetu. Ikanilazimu kumnunulia Fredy kama nilizo vaa, pamoja na simu inayo fanana na mimi. Nikatafuta laini mpya ya kuwasiliana na Fredy tu, kwani ya kwangu imeunganishwa na namba ya mama.

"Bado nini hapa"

"Sweta ulilo vaa wewe"

"Twende nitakupa mbele ya safari"

  Tukaingia kwenye gari ya Smith, tukaelekea nyumbani kwetu, ambapo nikakuta basi kubwa, lililo toka kuwachukua ndugu kutoka stendi ya ubungo, walio toka mikoa tofauti kuja kushuhudia harusi yangu, wakishuka na kuingia ndani, huku wengine wakicheza kwa furaha.

Nikampa Fredy sweta langu na kujifunika kichwa chake, akajichanganya na wanandugu hao, walio landuka kwa kucheza kwa furaha, wengine wakionekana kulewa chakari. Fredy akafanikiwa kuingia ndani pasipo kustukiwa. Nikampigia simu

"Sasa chumba chako ni kipi?"

"Si umeona kuna nyumba tatu?"

"Ndio"

"Sasa wewe, pandisha kwenye hilo gorofa lenye rangi ya pinki, achana na hayo majengo mawili yenye ghorofa mbili mbili"

"Mbona zote zina rangi sawa"

"Hilo jengo la katikati, ndio upande, si umeliona?"

"Ndio naelekea"

Smith akawasha gari, tukaondoka, huku simu yangu ikiwa hewani

"Nipo ndani"

"Pandisha ngazi hizo utakuta kirdo ndefu, nyoosha hadi mwisho chumba cha mwisho kushoto ndio changu"

Japo ni jambo la hatari tunalo lifanya mimi na Fredy ila hapakuwa na njia nyingine zaidi ya kufanya hivyo.

"Nimesha ingia chumbani kaka, nipazuri sana"

"Sasa kazi kwako, ila hakikisha huwi muongeaji sana, usije ukachapia baadhi ya vitu"

"Nimekupata, demu anaitwa Sheila?"

"Ndio"

"Poa, kaka kukiwa na shida nitakueleza"

"Sawa"

Moja kwa moja tukaelekea Mbagala, hadi nyumbani kwa Fredy, kutokana Smith anapafahamu haikuwa shida kwangu kupajua. Tayari yaamekatika masaa manne yamesalia masaa kumi na moja kabla sijapeleka pesa ya kumkomboa Phidaya na mwanangu Junio.

Kitendo cha kushuka kwenye gari, nakastukia nikiguswa kwa nyuma, kugeuka nikakutana na Manaka akiwa amejitanda kanga mbili mwilini mwake