SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 4 Novemba 2016

T media news

MASTER J AFUNGUKA UKIMYA WAKE KWENYE GAME YA BONGO

Producer Master J ameamua kufunguka juu ya kuwa kimya katika Industry ya muziki.

Baada ya kuamua kuachana na indusrty nzima ya muziki wa bongo tangu mwaka 2008 na kustaafu, Master J amesema kwamba chanzo ambacho kimemfanya kuacha muziki na kuendelea ishu nyingine ni kutokana na kuona kwamba soko la maproducers limejaa watoto ambao wanatoa ngoma bure.

“Album ya mwisho kuifanya ilikuwa 2008, baada ya hapo nikastaafu. Niliona niache niendelee na biashara nyingine, niliona soko la ‘Producers’ limejaa watoto, niseme ukweli tu. Producers wengi sasa wanatoa ‘Beat’ bure, tulishafika wakati tunarekodi kwa Milioni halafu turudi tena kurekodi kwa laki! Alisema Master J

Master J aliongeza kusema kwamba mpaka sasa wasanii wa muziki ndio wanamiliki magari ya kifahari na nyumba nzuri ila ukija kwa maproducer unakuta hakuna chochote kile.

‘Nitajie jina la producer hapa bongo anae-drive gari la zaidi ya Milioni 20.. Hakuna wote ni milioni 6 hapo! Wasanii wanapita na magari ya kifahari, wana nyumba za maana huku producers hawana chochote. Kifupi muziki umebadilika sana. Acha tufanye mambo mengine ya kifamilia sasa hivi.” Alimaliza Master J