NYOTA wa sinema za Bongo, Issa Mussa ‘Cloud’ amefunga ndoa tena, lakini safari hii ni kwa siri huko nchini Sweden na mwanamke aliyetajwa kwa jina moja la Mina ambaye amekuwa akimposti kila kukicha mitandaoni kwa kumuita pacha.
Chanzo kilicho karibu na staa huyo kililiambia gazeti hili kuwa, Cloud amemfanyia mbaya mkewe, Cynthia kwa kuamua kuoa kwa siri wakati imani yake inamruhusu kuwa muwazi.
Chanzo kilisema kuwa, awali Cloud alimwambia mkewe wa Bongo kuwa, amepata mfadhili hivyo anakwenda nchini Comoro kupata matibabu ya moyo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu, kumbe haikuwa hivyo bali alikwenda Sweeden ambapo yupo na mwanamke huyu anaedaiwa kufanya kazi ya uuguzi huko...mkwewe Cloud baada ya kusikia nyeti hizo kwa sasa amerudi nyumbani kwao.....
Chanzo kilicho karibu na staa huyo kililiambia gazeti hili kuwa, Cloud amemfanyia mbaya mkewe, Cynthia kwa kuamua kuoa kwa siri wakati imani yake inamruhusu kuwa muwazi.
Chanzo kilisema kuwa, awali Cloud alimwambia mkewe wa Bongo kuwa, amepata mfadhili hivyo anakwenda nchini Comoro kupata matibabu ya moyo ambao umekuwa ukimsumbua kwa muda mrefu, kumbe haikuwa hivyo bali alikwenda Sweeden ambapo yupo na mwanamke huyu anaedaiwa kufanya kazi ya uuguzi huko...mkwewe Cloud baada ya kusikia nyeti hizo kwa sasa amerudi nyumbani kwao.....