SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 24 Novemba 2017

T media news

SIMULIZ; MTOTO WA BOSS WANGU


Mtunzi: Bikora saidy
Contact: 0742754991

SEHEMU YA KWANZA ( 01)

Kuna msemo usemao usilolijua litakusumbua sana na ukilijua utatuzi wake hauhitaji nguvu sana maana itakuwa vyepesi kulikwepa au kuendana nalo

Hii lilidhihirika kwa kijana Wangesi mtoto wa mzee Kamau aliyejikuta akiangukia katika dimbwi la maisha magumu sana na hakujua kipi cha kufanya ili aweze kutatua hali yake maana mzee wake alianza kumdai hela yake baada ya kufeli kidato cha nne

 Huko nyumbani kwao kumbuka kuna watoto wengine husoma kwa shida sana na mzazi kupata ada ya kulipia inakuwa ni changamoto sana!

Wangesi alisoma kwa shida sana alikuwa ni mtu mwenye ndoto zake za kufika mbali sana alitamani kufika chuo kikuu akiamini kuwa kufika huko ndio maisha yatakuwa yamenyooka alilia sana alipokuwa akiwaona wanavyuo wakivaa joho zao

Huku akitamani na yeye awe miongoni mwao  lakini hali ngumu ya maisha nyumbani kwao ilimfanya ashindwe kuendelea na shule hali ya kuwa alimaliza kidato cha nne hakufanikiwa kuendelea na shule baada ya kuwa na wastani mdogo wa ufaulu.

Wangesi aliyachukia sana maisha yale magumu nyumbani kwao kitu kilichomfanya azame katika kufanya kazi kwa nguvu zote maana aliamini kuwa shule hawezi kuendelea tena kulingana na ufaulu wake kuwa mdogo sana alianza kulima bustani ya matunda pale nyumbani kwao

 Ambapo aliamini kuwa ndio mkomboz pekee wa maisha yake kwa muda ule alipenda sana kazi zake ziende mbele na sio kuwa mvivu hakika kijana wangesi alipenda sana kujishugulisha aliendelea na kazi ile kwa muda wa miaka kadhaa ubize wake ulimfanya kusahau kuwa duniani kuna jinsia ya kike

 Alishinda kwenye kazi zake na aliwaeza kuwakumbuka kuwa kuna jinsia ya kike mara alipokuwa akikutana nao alikuwa kujana mweusi kiasi na mwenye sura ya duaru alikuwa mfupi japo sio sana na mwenye umbo la miraba minne alijazia kifua chake sana

 Aisee mabinti wengi walipagawa na uchapakazi wa kijana wangesi mtoto wa mzee Kamau kila alipokuwa akipita aliacha maswali kwa watoto wa kike huku wakijiuliza kama ameoa au bado na kama hajaoa mchumba wake niyupi?

Ni baadhi ya maswali waliyokuwa wakijiuliza pale tu alipokuwa akikatiza Wangesi

Wengine walidiriki kusema huwenda jogoo hawiki ndio maana hapendi wanawake

Wangesi alipopat habari hizo hakuweza kujali maneno aliweza kuendelea na kazi zake muda wote!.

Baada ya miaka kadhaa Wangesi aliweza kutimiza kiasi cha fedha alichokuwa akikihitaji lengo lake ilikuwa kuendelea na shule baada ya kupata kiasi hicho wangesi aliweza kutafuta shule ya ufundi ambapo aliweza kwenda kusomea udereva na utengenezaji wa magari ( machenica)

Aliweza kutafuta chuo hicho na mwisho wa siku aliweza kupata alilipia ada ya mwaka mmoja na alianza masomo yake muda huo chuoni pale kwa Mara ya kwanza alipata shida sana maana mazingira aliyaona magumu lakini baada ya siku kadhaa aliweza kupata marafiki maana yeye alikuwa mkimya sana hivyo alipendelea sana marafiki ambao sio walopokaji

Alitulia sana mwisho wa siku akampata rafik wa kike  aitwae Sarah
Sarah alianza kujiweka kwa wangesi muda wote alijitahidi sana kuwa karibu yake hapo kusoma kwao kuliendelea kuwa katika hali nzuri ya upendo na heshima ilitawala katikati yao

Wangesi hakupenda utani sana katika suala la kitu cha maana alipenda afanye kitu na kiende alivyopanga na sio kupindisha Sarah nae aliweza kumuelewa wangesi kipi anapenda na kipi hapekut
Maisha yaliendekea na shule ilikaribia kufika ukingoni huku Sarah akijiuliza hivi wangesi jogoo anawika au hawiki?

Usikose sehemu ya 2 ndio kwanza simulizi imeanza kura yako ndio itakuwa mwendelezo wa simulizi hii hakika mtaipenda sana maana story nimetulia katika uandishi wake!!