SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 19 Machi 2017

T media news

Diamond Afungua Mwaka na Deal Hii Kubwa ya Ubalozi...!!!



Msanii wa muziki Nassib Abdul maarufu, Diamond Platnumz ameteuliwa rasmi na kampuni ya GSM kuwa balozi wa kutangaza bidhaa mbalimbali za taasisi hiyo.

Akizungumza Jijini Dar es Salaam Afisa Masoko wa kampuni hiyo, Lauma Mohamed ameeleza kuwa Diamond

Platnumz ni msanii mkubwa sana ndani na nje ya Afrika, hivyo wanaimani atakuwa balozi mzuri kwa bidhaa zao

bora kwa watanzania.

Kwa upande wake Diamond Platnumz ameeleza kuwa anafarijika sana kuona wasanii watanzania wanapata nafasi

ya kuwa mabalozi, kwani wasanii ni wengi lakini yeye amepata heshima hiyo hivyo ana imani ni jambo jema kwa tasnia ya muziki.

Ameongeza kuwa hapo mwanzo bidhaa nyingi kwa mfano samani za ndani zilikuwa zinaagizwa nje ya nchi lakini kwa

sasa itakuwa rahisi kwani GSM kwenye duaka lao la ‘The New Home’ wanauza samani hizo halkadhalika nguo za watoto.

Licha ya kumtambulisha msanii huyo kama balozi mpya wa GSM wamezindua matangazo mapya mawili yaliyoigizwa na msanii

huyo pamoja na familia yake akiwemo Zari the Boss Lady na mtoto wao Tiffa, huku tangazo moja likiwa la nguo na lingine la samani za ndani.