Serikali ya Ukraine imesema imepokea maombi kutoka kwa nchi 11 za Mashariki ya Kati na Ulaya zinazotaka msaada wa kiusalama ili kukabiliana na mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) za Iran.
Rais wa Ukraine, Volodymyr Zelenskyy, alisema nchi hizo zinaonesha nia kubwa ya kujifunza kutokana na uzoefu wa Ukraine katika kukabiliana na mashambulizi ya droni wakati wa vita.
“Kuna hamu kubwa ya kujifunza kutoka kwa uzoefu wa Ukraine katika kulinda maisha ya raia, matumizi ya mifumo ya kuzuia mashambulizi, teknolojia za vita vya kielektroniki pamoja na mafunzo ya kijeshi,” alisema.
Zelenskyy aliongeza kuwa Ukraine iko tayari kushirikiana na kutoa msaada kwa nchi hizo, hasa zile zinazosaidia kulinda maisha ya wananchi wa Ukraine na kudumisha uhuru wa taifa hilo.
