SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 1 Septemba 2017

T media news

Lusekelo Anthony 'Mzee wa Upako' Atoboa Siri...Adai Mwanaume Ukifanya Hili Kwa Mwanamke Hata Kaa Akuache

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo-Kibangu jijini Dar es Saalam, Lusekelo Anthony 'Mzee wa Upako' amefunguka na kuwashauri wanaume kuwa katika vitu ambavyo vinajenga ndoa na kuimarisha ndoa ni pamoja na mwanaume kuwa na makazi ya kudumu.

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) Ubungo-Kibangu jijini Dar es Saalam, Lusekelo Anthony 'Mzee wa Upako

Mzee wa Upako alisema hayo alipokuwa kwenye kipindi cha UJENZI kinachoruka kila Jumapili na kusema wanawake wanaojitambua na kujiheshimu tofauti na wale wasiojitambua na kujielewa basi wanaweza kumuheshimu sana mwanaume pindi mwanaume huyo anapojenga nyumba na kuwa na mji wake wa kudumu.