Baada ya Ally Yanga kufariki, kuna jamaa ameibuka na kuamua kubeba jukumu la kuvaa uhusika wa Ally Yanga, Mark Yanga ameonekana kwenye mechi ya Ndondo Cup akiwa katika mwonekano tuliozoea kuuona kwa Ally Yanga enze za uhai wake wakati alipokuwa akiishangilia Yanga na timu za taifa.
Dauda TV ilipata fursa ya kupiga story na Mark Yanga ambaye ameeleza sababu za yeye kuamua kuvaa viatu vya Ally Yanga lakini pia ameomba wana Yanga wampe ushirikiano ili aweze kuliziba pengo la kipenzi chao Ally Yanga.
Swali kubwa linaloulizwa ni kwamba, Mark Yanga atatosha kwenye viatu alivyokuwa akivivaa Ally Yanga?