SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 4 Mei 2017

T media news

Rais Magufuli Ateua Mkurugenzi Mkuu wa TBS

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Egid Beatus Mubofu kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS).

Taarifa iliyotolewa leo tarehe 04 Mei, 2017 na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi imeeleza kuwa uteuzi wa Prof. Egid Beatus Mubofu umeanza tarehe 02 Mei, 2017.

Prof. Egid Beatus Mubofu aliyekuwa akikaimu nafasi hiyo amechukua nafasi iliyoachwa wazi na Bw. Joseph B. Masikitiko ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Gerson Msigwa.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
04 Mei, 2017