Bunge la Tanzani leo limepiga kura na kuwachagua wabunge wawili wa CHADEMA watakaoungana na wenzao 7 kutoka CUF na CCM kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika Bunge la Afrika Mashariki (EALA).
Uchaguzi huo wa wabunge wa CHADEMA umerudiwa leo baada ya wagombea wa kwanza kukataliwa bungeni kwa kupigiwa kura ya hapana kwa kile kilichoelezwa kuwa hawakuwa wamekidhi vigezo.
Katika uchaguzi wa leo, wabunge wawili waliochaguliwa ni Josephine Sebastian Lemoyan na Pamela Pamela Maasay.
Katika kinyang’anyiro hicho wagombea wengine walikuwa nia Ezekiel Wenje, Lawrence Masha, Salum Mwalimu na Prof. Safari.
Kufuatia ushindi wa wagombea hao wawili, wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki sasa wanafikia 9 ambapo 5 ni wanawake na 4 ni wanaume.
Wabunge tisa wa Tanzania katika Bunge las Afrika Mashariki ni;
Fancy Nkuhi (CCM)Happiness Legiko (CCM)Maryam Ussi Yahya (CCM)Dkt Abdullah Makame (CCM)Dkt Ngwaru Maghembe (CCM)Alhaj Adam Kimbisa (CCM)Habib Mnyaa (CUF)Josephine Sebastian Lemoyan (CHADEMA)Pamela Pamela Maasay (CHADEMA).
Matokeo : Kura zilizopigwa 296
Kura halali 296
Abdallah Safari 35
Wenje 34
Josephine Lemoyan 219
Lawrence Masha 44
Pamela Maasay 200
Salim Mwalimu 59
Hayo ndo matokeo
Mshindi ni Josephine Leyamon