SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 6 Novemba 2016

T media news

Arsenal Kukabiliana na Tottenham Leo.


Mesut Ozil amefunga mabao matano.

Arsenal wanatumai kwamba beki wa kulia Hector Bellerin atakuwa tayari kushiriki huku Theo Walcot pia naye akifanyiwa ukaguzi wa iwapo yuko tayari.

Nacho Monreal,Kieran Gibbs na Santi carzola hawajaulikani iwapo watacheza lakini Granit Xhaka anarudi baada ya kuhudumia marufuku ya mechi tatu.

Mshambuliaji wa Tottenham Harry Kane atarudi baada ya kuuguza jereha la kifundo cha mguu ,lakini bado hajajiandaa kwa mechi hiyo.

Moussa Sissoko anahudumia marufuku ,huku Ben David ,Erik Lamela na Toby Alderwiereld wakiwa na majeraha.

Mousa Dembele huenda asicheze kutokana na jeraha la kifundo cha mguu.