SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumanne, 13 Septemba 2016

T media news

Rouhani agoma kukutana na Obama

Tehran, Iran. Vyombo vya habari nchini Iran vimemnukuu Makamu wa Kwanza wa Rais wa nchi hiyo, Es’haq Hahangiri akisema Rais Hassan Rouhani hana mpango wa kukutana na Rais Barack Obama wa Marekani wakati wa mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.

Mkutano huo wa baraza kuu unatarajiwa kufanyika mwaka huu mjini New York, huku viongozi mbalimbali wa dunia wakihudhuria.

Rais Rouhani atahudhuria mkutano huo akiongozana na Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Mohammad Javad Zarif