SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 20 Mei 2016

T media news

SUPER STAR LADY JAY DEE KUMUANIKA MRIDHI WA GARNER LEO

Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee au Jide’

Stori:  Andrew Carlos, Ijumaa

Dar es Salaam: Exclusive! Lejendari wa Bongo Fleva kwa zaidi ya miaka kumi na tano, Judith Wambura Mbibo ‘Lady Jaydee au Jide’, anatarajia kumuanika mrithi wa aliyekuwa mumewe, Mtangazaji wa Kituo cha Radio CloudsFM, Gardner G. Habash ndani ya saa 24, Ijumaa lina data kamili.

Kwa mujibu wa habari za kuaminika zilizothibitishwa na uongozi wa staa huyo, Jide atamtambulisha mchumba wake huyo kwa mara ya kwanza ndani ya Ukumbi wa Mlimani City leo, Dar ambapo pia atafanya shoo ya saa tatu mfululizo, inayokwenda kwa jina la Naamka Tena.