SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumamosi, 19 Machi 2016

T media news

Ommy Dimpoz: Naahidi kumtambulisha msanii mmoja kutoka PKP mwaka huu

Jay Z aliona mbali akaamua kuanzisha lebo yake ya Roc Nation ambayo imekuwa kubwa kwa sasa na inawasimamia mpaka mastaa wakubwa Marekani wakiwemo Rihanna na J-Cole.

Muziki wa Tanzania unaelekea kukua zaidi kutokana na mastaa kibao kuanzisha lebo zao kuwasaidia wasanii wanaochipukia.

Akizungumza na kipindi cha Friday Night Live, kinachoruka kupitia EATV, Ommy Dimpoz alisema mwaka huu atamtambulisha msanii mmoja kutoka lebo ya PKP.

“Baada ya kuanzisha lebo yangu ya PKP, naahidi mwaka huu kumtambulisha msanii wangu mmoja. Najua watu wataanza kusema kuwa mpaka fulani aanzishe na wewe ndio uige, wanasahau kuwa nilitangaza muda kuwa nimeanzisha lebo yangu.”