SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 11 Aprili 2019

T media news

Rais Magufuli Awaonya Wanaosambaza Pembejeo HEWA



“Nilipoingia madarakani niliahidi nitakuwa daktari wa kutumbua majipu zikiwemo hizi hewa ili fedha halali zitumike katika masuala mengine halali, ninajua wapo waliopata pembejeo za haki na tukishamaliza ufuatiliaji wa pembejeo watalipwa,” amesema.

Aidha amewapongeza wakazi wa Mkoa huo kwa ujenzi mzuri wa nyumba ambapo ameitaka mikoa mingine kuiga mfano huo kwa kujenga nyumba nzuri na za kisasa.

“Tangu nimeingia Njombe nimeona nyumba zilizojengwa ni tofauti na nyumba zilizonyengwa huko kwetu kwani hakuna nyumba ya majani zote ni za bati na zimejengwa kwa matofali ya kuchoma ninafikiri mikoa mingine ambayo haijabadilika katika ujenzi wa nyumba waje wajifunze huku,” amesema Dk Magufuli.