SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 7 Agosti 2016

T media news

RIWAYA: Sorry Madam - Sehemu ya 11 & 12



MTUNZI:EDDAZARIA G.MSULWA

.....Maumivu makali yakanitawala katika kifua changu nikajishika kwenye kifua changu na kugungua kuna damu zinanitoka ikanibidi niukaze mkono wangu ili kuzuia damu nyingi kuendelea kuvuja katika sehemu risasi ilipo pita.Manka akaanza kuweseka huku akiwa kama haamini kwa tukio alilo lifanya.Akaitupa bastola chini na kupiga magoti kuangalia eneo aneo alilo nijeruhi kwa risasi

“Eddy nilikuwa ninakutania”

Manka alizungumza huku akilia na kuonekana kuchanganyikiwa kwa kitendo alicho nifanyia.Taratibu nikahisi nguvu zikiniishia huku mwili ukizizima kwa kukosa uwezo wa kufumbua machona taratibu nikajikuta hali nzito ambayo sikuwahi kuipata katika maisha yangu ikiutawala moyo wangu.

                                     

 Macho yangu yakafunguka na kujikuta Mama akiwa amekaa pembeni yangu huku puani kwangu nikiwa na mashine ya kupulia.Mama alipo niona nimefungua macho yangu akaanza kuliita jina langu na nikamuitikia kwa sauti ya chini

“Mwanangu unajisikiaje?’

Nikataka kunyanyuka ila nikashindwa na mama akanirudisha chini na kugundua kuna bandeji kuwa nimefungwa kwenye kifua changu.Kumbukumbu zinanikumbusha dakika za mwisho nilikuwa na Manka ila kuanzia hapo sikuelewa kitu kilicho enedelea hadi mama akawa pembeni yangu.

“Mama nipo wapi?”

“Mwanangu upo hospitalini?”

“Nani kanileta?

“Ni story ndefu kidogo mwanangu ila kwa sasa pumzinka nitakuadisia ukipata nafuu”

   Simu ya mama ikaita akaitazama kwa muda kisha akaipokea na nikamuona sura yake ikiwa imebadilika kidogo na kuwa sura ya hasira

“Ndio ameamka”

“Godwin nakuomba unielewe hapa huna mtoto na huyo mwanao aliye mfanyia mwanangu hivi nilazma nimfunge”

“Ahhhh kwahiyo wewe ndio umemtuma amuue mwanangu si ndio?”

“Sasa lazima nimfunge na kumbuka kuwa tangu mwanangu akiwa utotoni hukuwa na mapenzi naye sasa naomba umuache na wala sihitaji urudi uje umuuone”

 Mama akakata simu huku akiachia msunyo mkali,sasa sikuelewa anazungumza na nani na kumfokea kiasi hicho

“Mama unazungumza na nani?”

“Ahaaa mwanangu nitakuambia”

Mama alanijibu huku akiwa anatabasamu kisha akanibusu katika paji la uso wangu.Simu yake ikaiita tena na ikamlazimu kutoka nje.Sikutaka kujisumbua mama anamfokea nani niahisi watakuwa ni watu wa serikali anao fanya nao kazi.Mama akarudi na kukaa karibu yangu huku machozi yakimlenga lenga akionekana kuwa na hasira kubwa na tangu nizaliwe sikuwahi kumuona mama akiwa katika hali kama hiyo.

“Mama nipo hospitali gani?”

“Ni KCMC”

 Mlango ukafunguliwa akaingia mzee wa makamo akiwa amevalia nguo za polisi huku akiwa na vyeo vingi

“Habari yako mheshimiwa?”

“Salama vipi mumesha mkamata aliye sababisha hili tukio?”

“Ndio muheshimiwa ila ninashindwa kuelewa kwani mzee ananiambia nimuachie huru ili we……”

“Nisikilize wewe mimi si ndio nimetoa  amri yule binti kukamatwa?”

“Ndio”

“Sasa mbona unaniletea Kiswahili.Muwekeni ndani hadi mimi nije sawa”

“Sawa mkuu”

Askari akatoka na kutuacha ndani ya chumba na ukimya ukatawala huku mama akonekana kusongwa na mawazo na mara kwa mara akawa anasunya sikujua kinacho mfanya asunye ni nini.

 Nikakaa hospitali kwa wiki moja nikapewa ruhusa japo sikuwa nimepona vizuri.Safari ya kwenda uwanja wa ndege wa KIA ikaanza huku dereva anayemuendesha mama akiwa makini katika uendeshaji wake kutokana Dokta ameniambia nisifanye kazi ngumu wala kupata mitingishiko ya aina yoyote kwani kidonda changu kinaweza kisipone kwa haraka.Tukakuta ndege ya kukodi ikiwa tayari kwa ajili yetu mimi na mama.Tukapanda na dereva akaondoka na gari ya mama na tukaahidiana naye atatukuta nyumbani.Safari ikaanza taratibu huku ndege aina ya Fast Jet tuliyoipanda ikizidisha kasi kadri muda unavyo kwenda tukiwa angani

  “Pole kaka”,Muhudumu wa kike wa ndege akanipa pole huku akiniwekea juisi kwenye kimeza kidogo kilichopo mbele yangu

“Asante”

“Muheshimiwa huyu ni mwanao”

“Ndio ni mwangu wa kwanza na wamwisho”

“Aisee mtu akikutizama wala hata amini kama unamtoto mkubwa kiasi hichi”

“Unajua kipindi sisi tulipokuwa tunamaliza kidato cha sita mika ya themanini tulipelekwa jeshini sote na ilitusaidia kuweza kuzilinda afya zetu ni tofauti na hao kina Eddy mtu nikimwambia mwanangu ana miaka 20 haamini”

“Mmmm mama umekosea nina miaka 21”

“Sasa sibado haijatimia”

“Sasa muheshimiwa nyinyi si mupo huku ngazi za juu kwanini musirudishe sheria ya wanafunzi wanao maliza kuingia jeshini?”

“Ile imerudishwa sasa sijui huku mwanagu kama ataweza kwa maana mmmm”

“Mama wewe unaniona mimi nimeoza sana”

“Wewe hujioni”

Tukacheka sote na safari ikaendelea,haikuchukua muda sana kutua katika uwanja wa ndege wa mwalimu JK Nyerere.Gari ya serikali ikaja kutuchukua na kutupeleka nyumbani maeneo ya Masaki.Nikakumbuka kuna kitu ninakihitaji kukijua vizuri kutoka kwa mama kwani kila nilipohitaji kumuuliza nilijikuta nikisahau

“Mama hivi pale hospitalini nilifikaje?”

“Eddy mwanagu hata hatujapumzika umeanza kwa maswali?”

“Ndio ama nataka kujua?”

“Kavue nguo zako chumbani kwako upumzike kisha wakati wa jioni tutazungumza ngoja mimi niende ofisini jana kuna kazi niliiacha”

“Kwani mama jana ulikuja ofisini?”

“Ndio kila siku nilipokuwa ninakuja hospitali nilikuwa ninalala Dar asubuhi ninakuja kwa ndege jioni au mchana ninarudi kwa ndege”

“Mmmmm mama mbona nyumba ipo kimya dada wa kazi yupo wapi?”

“Nimemfukuza”

“Kwa nini?”

“Nitakuja kukuambia jioni nikitoka kazini”

Mama akaondoka mimi nikaelekea chumbani kwangu,sikukuta kuna mabadiliko ya aina yoyote tangu nilipo kiacha pindi nanakwenda shule.Nikaingia bafuni nichukua taulo na kulichovya kwenye maji na kuanza kujisujgua sehemu ya mwili kwani ndio oga yangu tangu nikiwa huspitalini hii ilisaidia kidonda kuto kuingia maji.Nikamaliza na kurudi kitandani kutokana nimeshiba nikaamua kulala...