SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 24 Machi 2016

T media news

Shirika la UmemeTanzania linawataarifu wateja wake kuwa kutakuwa kuna maboresho katika mfumo wake wa LUKU

Shirika la  UmemeTanzania

Taarifa kwa Umma
Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO) linawataarifu wateja wake kuwa kutakuwa kuna maboresho katika mfumo wake wa LUKU utakapopelekea wateja kushindwa kununua Umeme siku ya Alhamisi tarehe 24, March 2016 kuanzia saa 5 usiku hadi tarehe 25 March, 2016 saa 11 Alfajiri.

Sababu za kukosekana kwa huduma hiyo ni : Matengenezo ya kuboresha mfumo wa Luku.

Uongozi unaomba radhi kwa usumbufu utakaojitokeza.

Imetolewa na ofisi ya uhusiano TANESCO makao makuu.