SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 20 Aprili 2018

T media news

Hiki ndicho chanzo cha ukosefu wa nguvu za kiume

Ukosefu nguvu za kiume katika karne hii ya ishirini na moja imekuwa ni tatizo kubwa ikilinganishwa na  kipindi cha zamani, halikadharika tatizo hili limekuwa likisababisha kuendelea kwa michepuko kila kukicha hata kupelekea ndoa na mahusiono mengi ya kimapenzi kufa.

Na maana halisi ya upungufu wa nguvu za kiume ni; Ukosefu ama upungufu wa nguvu za kiume ni ile hali ya mwanaume kutokuwa na uwezo wa kukamilisha tendo la ndoa kwa ufasaha.

Mwanaume mwenye tatizo la ukosefu ama upungufu wa nguvu za kiume anakuwa hana uwezo wa kumtosheleza mwanamke kwenye tendo la ndoa. Baade mwanamke baada ya huona hali hiyo huamua kwenda kwa mwanaume mwingine ambaye ana uwezo wa kukidhi matakwa yake ya kimapenzi husasani swala zima la tendo la ndoa.

Chanzo cha ukosefu wa nguvu za kiume ni kama ifuatavyo;

(a) Upigaji punyeto wa muda mrefu.
(b) Woga wa kufanya tendo la ndoa.
(c) Msongo wa mawazo.
(c) Ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu (pressure).
(d) Kupooza kwa mwili.
(c) Kuugua ugonjwa wa ngiri.
(d) Kuugua chango la kiume.
(e)Ulevi uliokithiri.
(f)Ulaji mbovu wa vyakula haswa vyenye mafuta mengi/kupita kiasi.
(g)  Mazingira yasiyoridhisha wakati wa tendo la ndoa.