SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatano, 14 Machi 2018

T media news

Manchester United Yatolewa Kwenye Michuano ya Champions League

MAN United baada ya kufungwa bao 2-1 wametolewa na Sevilla usiku wa kuamkia leo  wametolewa kwenye michuano ya Champions League.

Hakuna aliyetaraji kutokana na uwezo mkubwa wa United na rekodi mbovu ya Sevilla nchini Uingereza lakini tangu dakika ya kwanza mpira ulianza kuonekana kama unawaelemea United walikua wakicheza kawaida sana.

Mchezo mwingine uliopigwa usiku huu Eden Dzeko aliivusha As Roma kwenda robo fainali baa ya kufunga bao pekee mbele ya Shakhtar Donetski, Roma wamefudhu kwa faida ya bao la ugenini.