SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 7 Septemba 2017

T media news

Zitto Kabwe: Watanzania Tuungane Pamoja Kupinga Siasa za Mauaji

Mbunge wa jimbo la Kigoma Mjini Mhe. Zitto Zuberi Kabwe amewataka wananchi kusimama imara na wasikubali kabisa kuruhusu siasa za mauji kupata nafasi nchini Tanzania.

Zitto ameeleza hayo kupitia ukurasa wake wa facebook mara baada ya kutokea taarifa ya kupigwa risasi kwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Antipas Lissu na watu wasiyofahamika.

"Nchi yetu imefungua ukurasa mpya. Wananchi tusimame imara tusikubali kabisa kuingia kwenye siasa za namna hii. Mola amponye ndugu yetu",ameandika Zitto.

 Mhe. Tundu Antipas Lissu amepigwa risasi kadhaa mwilini mwake akiwa nyumbani kwake Dodoma eneo la 'area D' na watu wasiojulikana