SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 7 Septemba 2017

T media news

Chemical Akana Kumpenda Sterio

RAPA wa kike anayefanya vizuri kwenye Hip Hop Bongo, Claudia Lubao ‘Chemical’, amefunguka kuwa, msanii Stereo ambaye amekuwa akijanasibu kwenye vyombo vya habari kwamba anampenda, ukweli ni kwamba mwanamuziki huyo hajawahi kumpenda
kwa dhati kwa kuwa bado mwanaume huyo hajamwonesha vitendo vyenye kuthibitisha hilo.

Chemical alisema kuwa, hajawahi kupendwa kwa dhati na Stereo kwa kuwa hata siku moja, hajawahi kuelezwa kitu chochote kinachohusu mapenzi na rapa huyo, zaidi ya kumsikia tu kwenye vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

“Siwezi kujiongopea kwamba nimewahi kupendwa na Stereo, hata mara moja rapa huyo hajawahi kunipenda, nasema hivyo kwa sababu hajawahi kunifungukia live, ninaishia kumsikia tu kwenye media na mitandao ya kijamii,” alisema Chemical.