Usiku wa kuamkia leo majira ya saa mbili ajali nyingine imetokea katika kijiji cha Lusanga-Muheza ambapo gari aina ya coaster inayofanya safari zake Tanga-Lushoto imegonga lori kwa nyuma,na kusababisha vifo vya watu wanne.
Kwa mujibu wa taarifa za awali kutoka eneo la tukio zinaeleza kuwa Waliofariki kwenye ajali ya basi aina ya Coaster ni Wanne 4, wawili wanaume na wawili wanawake na
Majeruhi ni 15 ambao wamekimbizwa Hospital ya Teule Muheza kwa matibabu zaidi.