SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 17 Februari 2017

T media news

Taarifa za Mchekesha Kansime Kukamatwa na Madawa ya Kulevya London..Ukweli Huu Hapa

Kuna picha inasambaa kwenye mitandao kuanzia ikionyesha sehemu ya habari iliyoandikwa na mtandao uitwao METRO na inasema Mwigizaji/Mchekeshaji wa Uganda Anne Kansiime amekamatwa na Polisi kwenye uwanja wa ndege London akiwa na dawa za kulevya kilo mbili.

Ni habari zilizowashtua wengi lakini ukweli tumeupata, Anne hajakamatwa na yeye ni mzima wa Afya nyumbani kwao Kampala Uganda na usiku wa leo anatarajia kufanya show inayohusiana na sanaa yake.

Baadhi ya mitandao imekanusha na kusema kuwa sio kweli lakini pia baada ya hili nikapita kwenye ukurasa wa Instagram wa Anne kansime na kwenye picha ya mwisho kupost alicomment kusema yuko salama baada ya mwimbaji Irene Namubiru kumuuliza.


Kupitia ukurasa wake wa Twitter @Kansiime256 Anne aliandika pia kwamba kuwa yuko uwanja wa taifa Uganda tayari kwa show yake usiku wa leo.

"At the National Theatre Kampala, Uganda ready for tonight's show with my family @funfactory ......."