SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatano, 2 Novemba 2016

T media news

KUFURU LA PESA ONA WACHEZAJI 10 WANAOLIPWA PESA ZA AJABU HAPA DUNIANI LIVE!!


Licha ya Gareth Bale kusaini mkataba mpya na klabu ya Real Madrid utakaomuingizia kiasi cha Pauni milioni 108 katika miaka 6 ijayo, bado hawafikia kiwango cha kuwa mchezaji anayelipwa mkwanja mrefu zaidi duniani.

Rekodi hiyo imeendelea kushikiliwa na Cristiano Ronaldo na Lionel Messi wote wakisakata kabumbu nchini Uhispania.

Paul Pogba kutoka Manchester United ambaye ndiye mchezaji ghali zaidi duniani, ameshika nafsi ya 5 akitengeneza jumla ya Pauni 290,000 kwa wiki. Hii hapa chini ni orodha kamili ya wachezaji wanaolipwa fedha nyingi zaidi duniani.

1. Cristiano Ronaldo (Real Madrid) £365,000 kwa wiki, na £19m kwa mwaka.*

2. Lionel Messi (Barcelona) £365,000 kwa wiki, na £19m kwa 

mwaka.*

3. Gareth Bale (Real Madrid) £346,000 kwa wiki, na £18m kwa mwaka.*

4. Hulk (Shanghai SIPG) £317,000 kwa wiki, na £16.5m kwa mwaka.

5. Paul Pogba (Manchester United) £290,000 kwa wiki, na £15m kwa mwaka.

6. Neymar (Barcelona) £289,000 kwa wiki, na £15m kwa mwaka.*

7. Graziano Pelle (Shandong Luneng) £260,000 kwa wiki, na £13.5m kwa mwaka.

8. Wayne Rooney (Manchester United) £260,000 kwa wiki, na £13.5m kwa mwaka.

9. Zlatan Ibrahimovic (Manchester United) £250,000 kwa wiki, na £13m kwa mwaka.

10. Sergio Aguero (Manchester City) £240,000 kwa wiki, na £12.5m kwa mwaka.

10. Yaya Toure (Manchester City) £240,000 kwa wiki, na £12.5m kwa mwaka.

Wachezaji waliowekewa ‘*’ li wale ambao tayari wamekatwa kodi, ambapo hawana alama hiyo, fedha zao bado hazijakatwa kodi.