Rais wa Uganda, Yoweri Kaguta Museveni amekifunga kwa muda Chuo Kikuu cha Makerere kilichopo Kampala kufuatia vurugu zilizoibuka zikiwahusisha wanafunzi na wahadhiri wa chuo hicho.
Taarifa hiyo ya Rais Museven inaeleza kuwa, uamuzi huo una lengo la kulinda usalama wa watu pamoja na mali.
Mgomo huo ulianza baada ya wahadhiri hao kutaka kulipwa malimbikizo ya fedha ambazo hawajapewa kwa miezi 8 sasa. Baada ya wahadhiri hao kugoma kuanzia jana, leo Jumanne wanafunzi nao wakaungana nao.