SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatatu, 21 Machi 2016

T media news

FAIDA YA JUISI YA UKWAJU


Tunda la ukwaju ni tunda lenye faida nyingi sana kwa afya ya mwanadamu. Tunda hili huweza kutumika kutengeneza juisi ambayo matumizi yake yana faida kubwa sana katika afya ya mwili wa mwanadamu.

NAMNA YA KUTENGENEZA JUISI YA UKWAJU. 
Nunua ukwaju wako, ukwaju unapatikana kwa wingi sana masokoni na kwenye supermarkets
Andaa maji kwenye dishi na uoshe kidogo tuu   baada ya kuuosha chukua ukwaju wako weka kwenye sufuria yenye maji ya saizi na injika jikoni  uache uchemke kwa dakika 10/15 ili uuwe vijidudu

Ipua ukwaju wako jikoni na uache kwa muda upoe  andaa maji yako masafi na chujio ili uweze kuchuja juice yako kwa uangalifu zaidi ili upate juice yenyewe

Weka sukari kwa kiasi unachopendelea pia ili kupunguza ukali unaweza ukaweka hiliki au vanila ili kupata taste weka juice yako kwenye fridge ili ipoe tayari kwa kunywa.

FAIDA YA JUISI YA UKWAJU.

Chanzo kizuri cha viuasumu mwilini 'antioxidants' ambavyo huzuia Saratani (cancer)

Chanzo cha Vitamini B na C vile vile "carotentes"

Hushusha joto la mwili na kuondosha homa, hasa homa ya malaria na homa ya matumbo

Huulinda mwili dhidi ya mafua na kero za mafua kooni

Husaidia myeyusho na mmengenyo wa chakula na kuondosha kuvimbiwa

Husaidia kutibu matatizo ya nyongo (bile disorders)

Husaidia kurahisisha choo (laxative)

Husaidia kupunguza wingi wa lehemu (cholesterol) na hivyo kuimarisha moyo

Husaidia ngozi kuwa nyororo, vile vile husaidia ngozi inayopona baada ya kuungua au yenye
vidonda

Husaidia kuua minyoo tumboni (kwa watoto wadogo)