Mojawapo ya harusi ghali zaidi duniani imefanyika nchini India, na kugharimu jumla ya upee bilioni 5 ($74m; £59m).Harusi ya kifahari imefanyika jimbo la Karnataka, kusini mwa India na iligharimu karibu rupee bilioni 5 ($74m; £59m).
Harusi hiyo ya mfanyibiashara na mtoto wa mwanasiasa wa India G Janardhana Reddy's, Brahmani, imepokelewa kwa ghadhabu na mamilioni ya raia wa India ambao kwa sasa wanakumbana na matatizo ya kifedha.
Biarusi alikuwa amevalia sari iliyogharimu rupee milioni 170 ($2.5m; £2m) na akavalia mikufu iliyogharimu rupee milioni 900$13m; £10m), ripoti zimesema
Bwana harusi, Rajeev Reddy, 23, anayemiliki biashara ya familia yake kutoka mji wa Hyderabad.
Wachezaji wa ngoma ya Kibrazil ya Samba ni miongoni mwa waliowatumbuiza wageni kwenye harusi hiyo .
Watu wengine kwenye mitandao ya kijamii wamesema si vyema kuishtumu harusi hiyo. Bw Reddy amenukuliwa akisema alifanya malipo ya harusi miezi sita kabla harusi yenyewe - kabla serikali kuzifutilia mbali noti za zamani kama njia ya kukabiliana na ulaji wa rushwa - na aliweka mali yake rehani kwa ajili ya harusi.
Nyota wa Bollyhood waliowatumbuiza wageni kwenye harusi hiyo. Wakosoaji wamesema harusi hiyo ya kifahari ni 'kuonyesha utajiri'.
Maandalizi katika hekalu la Pangalore yalichukua miezi miwili kukamilika. Maandalizi yalifanyika na walitengeneza madhabahu mfano wa yaliyotumiwa na Wahindi wa kale kwa ajili ya harusi hiyo
Zaidi ya wageni 50,000 walihudhuria harusi hiyo. Ripoti zimesema teksi 2,000 ziliwabeba wageni na ndege aina ya helikopta 15 ziliwaleta wageni maalum waalikwa.