SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 18 Novemba 2016

T media news

CHECK PICHA HARUSI YA GHALI ZAIDI INDIA


JANARDHANA REDDY FAMILY

Mojawapo ya harusi ghali zaidi duniani imefanyika nchini India, na kugharimu jumla ya upee bilioni 5 ($74m; £59m).Harusi ya kifahari imefanyika jimbo la Karnataka, kusini mwa India na iligharimu karibu rupee bilioni 5 ($74m; £59m).


KASHIF MASOOD

Harusi hiyo ya mfanyibiashara na mtoto wa mwanasiasa wa India G Janardhana Reddy's, Brahmani, imepokelewa kwa ghadhabu na mamilioni ya raia wa India ambao kwa sasa wanakumbana na matatizo ya kifedha.


FAMILIA YA JANARDHANA REDDY

Biarusi alikuwa amevalia sari iliyogharimu rupee milioni 170 ($2.5m; £2m) na akavalia mikufu iliyogharimu rupee milioni 900$13m; £10m), ripoti zimesema


FAMILIA YA JANARDHANA REDDY

Bwana harusi, Rajeev Reddy, 23, anayemiliki biashara ya familia yake kutoka mji wa Hyderabad.


KASHIF MASOOD

Wachezaji wa ngoma ya Kibrazil ya Samba ni miongoni mwa waliowatumbuiza wageni kwenye harusi hiyo .


KASHIF MASOOD

Watu wengine kwenye mitandao ya kijamii wamesema si vyema kuishtumu harusi hiyo. Bw Reddy amenukuliwa akisema alifanya malipo ya harusi miezi sita kabla harusi yenyewe - kabla serikali kuzifutilia mbali noti za zamani kama njia ya kukabiliana na ulaji wa rushwa - na aliweka mali yake rehani kwa ajili ya harusi.


KASHIF MASOOD

Nyota wa Bollyhood waliowatumbuiza wageni kwenye harusi hiyo. Wakosoaji wamesema harusi hiyo ya kifahari ni 'kuonyesha utajiri'.


KASHIF MASOOD

Maandalizi katika hekalu la Pangalore yalichukua miezi miwili kukamilika. Maandalizi yalifanyika na walitengeneza madhabahu mfano wa yaliyotumiwa na Wahindi wa kale kwa ajili ya harusi hiyo


ALAMY

Zaidi ya wageni 50,000 walihudhuria harusi hiyo. Ripoti zimesema teksi 2,000 ziliwabeba wageni na ndege aina ya helikopta 15 ziliwaleta wageni maalum waalikwa.