SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 15 Februari 2018

T media news

TANGA RAHA- Sehemu ya Nne ( 4 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA

 ILIPOISHIA  

"Ngoja niondoke niende kuoga kisha nikarudi kuimalizia hii movie imenibamba sana"

Akatoka huku akilitingisha kalio lake kubwa ambalo kwenye tenge alilo livaa lilijitokeza vizuri na kuufanya mwili wangu kunisisimka

ENDELEA

Nikaufunga mlango wangu na kuingia bafuni nikanga nilipo maliza nikarudi kukaa kwenye sofa na kuanza kuandika topic(mada) nitakazo fundisha jumatatu nikiwa shuleni

Mida ya saa sita kasoro mlango wangu ukagongwa

"Nani?"

Ilinilazimu kuuliza kwani ni muda wa usiku na bado sikuwa mwenyeji katika mtaa huu

"Mimi mama Fatuma"

"Mama Fatuma yupi?"

"Mama yake mdogo Jumaa nimekuja kuimalizia ile movie"

Nikanyanyuka japo kwa tahadhari na kwena kuufungua mlango.Mama Fatuma akaingia huku akiwa amevalia suruali nyeusi iliyo mbana na kufanya hipsi zaka kupanuka vizuri na kalio lake kubwa kuchomoza zaidi ya nilivyo liona likiwa ndani ya tenge

"Karibu mwaya"

"Ile movie bado haijaisha?"

"Bado ila ndio ipo ukingoni kingoni"

Mama Fatuma akakaa kwenye sofa hapo ndipo nikapata muda wa kumtadhimini kuanzia usoni hadi chini.

Machn makubwa mazuri yaliyo legea kama mtu mwenye usingizi yanaendana na pua ndogo kiasi huku na midomo mipana ya wastani yenye meno meupe yaliyo jipanga vizuri.

Sura ya duara ya mama Fatuma ilizidi kumfanya kuwa mzuri zaidi.Macho yangu yakashuka hadi kifuani mwake ambapo kuna chuchu zilizo jalia ila zina ukubwa wa wastani zikazidi kuusisimua mwili wangu na kusabisha bastola yangu kusimama

"Labda nikupe kinywaji gani?"

"Una bia baridi?..Ila unaonekana wewe si mnywaji?"

"Nilikuwa ni mnywaji ila kama unahitaji ngoja nikakuchukulie"

"Sawa"

Nikampa rimoti ya Dstv ili hata akihitaji kubadilisha chanel abadilishe.Nikavaa vest na kutoka nje.Ila nikaufunga mlango wangu kwa nje ili hata kama atakuwa na lengo la kuniibia atashindwa

Kwa jinsi mtaa wa Chuda ulivyo na hotel na baa nyingi haikuwa ngumu mimi kutembea umbali umrefu kutoka na ninapo ishi.Nikanunua CARTON mbili za bia za kopo na mzinga mmoja wa VALUE

Kabla sijaondoka eneo la baa niliyopo nikaagizia nyama ya mbuzi ya kukaangwa kilo mbili na kurudi nyumbani.Nikamkuta Mama Fatuma akiwa amejilaza kwenye sofa huku taa akiwa ameizima