SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumatano, 21 Februari 2018

T media news

Idadi ya Watu Waliofariki kwa Kipindupindu Dodoma Ndani ya siku 150

Habari kutokea Dodoma zinaeleza kwamba Watu 20 wamefariki dunia mkoani humo kufuatia kuzuka kwa mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu kuanzia mwezi October mwaka jana wakati na wengine 471 wakiripotiwa kutibiwa hospitalini.

Kwa mujibu wa Mganga mkuu wa mkoa Dr James Kiologwe amesema idadi ya wagonjwa imezidi kuongezeka huku kwa siku ya jana pekee walipokea jumla ya wagonjwa kumi katika vituo vya afya na hospitali mbalimbali za mkoani humo .