SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumanne, 11 Aprili 2017

T media news

Simulizi ya Kusisimua: Kitanda cha Sokwe Mtu

Ni  simulizi  la  ukweli  linalo  husu  maisha  ya kijana  Lugwisha , kutoka  kitongoji cha  Goweko, wilayani  Uyui  mkoani  Tabora.

 Kijana  Lugwisha, baada  ya  kumaliza  shule  ya  msingi  mnamo  mwaka  1994 huko  kijijini  kwao, alifunga  safari  hadi  jijini  Dar  Es  Salaam, kwa  ajili  ya  kutafuta  maisha.

Miaka  kumi  baadae  , kijana  Lugwisha  akawa  amepata  mafanikio  makubwa  yaliyo badilisha  maisha  yake.

Mafanikio  katika  maisha  ya  Lugwisha  yanasababisha  kuinuka  kwa  maadui  ambao hawapendezwi   na  kufanikiwa  kwake.

Maadui  hawa  wanapanga  njama mbalimbali  za  kupambana dhidi ya  mafanikio  ya  Lugwisha.

Kati  ya  maadui  wa  Lugwisha,  ni  maadui  wawili tu  ndio wanaonekana  kuwa  na  nia thabiti  nay a  dhati  katika mapambano  dhidi  ya  Lugwisha.

Maadui  hao  ni  Beka  Msangi  pamoja  na  Bundala.

Beka  Msangi  alikuwa  mmiliki  wa  bar  iliyo  kuwa  jirani  na  bar  iliyo  milikiwa  na  Lugwisha.

Bar hii  ya  Lugwisha  ilikuwa  ni  moja  kati ya  makumi  ya  vitega  uchumi  vyake vilivyo  muingizia  fedha nyingi.

Bar ya  Lugwisha  ilikuwa maarufu  sana  jijini  Dar  Es  Salaam  na ilikuwa  ikifurika  wateja  kuanzia  Jumatatu hadi  Jumapili.

Bar  hii  ya  Lugwisha  ilikuwa  katika  eneo  lenye  bar  nyingi. Uwepo   wa bar  ya  Lugwisha  katika eneo  hilo uliua  biashara  ya  karibu  bar  zote  zilizo kuwepo  katika  eneo ikiwemo  bar ya  Beka  Msangi.

Beka  Msangi  hakutaka  kukubaliana  na  hali  hiyo  na hivyo  kufikia  uamuzi  wa  kusafiri  hadi  katika  kijiji  cha  Mchukwi  wilayani  Rufiji mkoani  Pwani,   kwa ajili ya  kumroga  Lugwisha.

 Baada  ya  kupiga  ramli, wachawi  wa Rufiji  wanaona  njia  pekee  ya  kupambana  na  Lugwisha  ni kumuhamisha  kichawi   yeye  na  bar  yake  kwa  kutumia  uchawi  wa  kizigua, ujulikanao  kama  “Sunkwa”.

Lengo  la skadi  hili  la  kichawi  lilikuwa  kumfanya  Lugwisha, yeye  mwenyewe  kwa  hiari  yake    afunge  bar  yake  katika  eneo  hilo  na  kuhamia  katika  eneo  jingine  na  wala  asipate  kabisa  wazo la  kurudi  tena  kufanya  biashara  katika  eneo  hilo,  hali  ambayo  ingemfanya  Beka  Msangi  aweze  kufanya  biashara  yake  ya  Bar  bila  ya  kupata  upinzani  wowote  mkubwa.

Ama  kwa  upande  wa  Bundala, huyu  ni  mdogo  wa  damu  wa Lugwisha.  Lugwisha  na  Bundala wamezaliwa  kwa baba  mmoja  lakini  mama  tofauti.

Baada  ya  kujaribu  kuomba  misaada  ya  mara  kwa  mara  kwa  Lugwisha  bila  mafanikio  yoyote, Bundala , mama  yake  ( ambae  ni  mama  wa  kambo  wa  Lugwisha  )  pamoja  na dada  yake  aitwae  Kalunde  ambae  alikuwa  Mwalimu  wa  shule  moja  ya  msingi  huko  mkoani  Kigoma, walijiridhisha  pasi  na  shaka  yoyote  kwamba, Lugwisha   anawadharua  sana  kwa  sababu  Mwenyezi  Mungu  amemjalia  fedha  na  mali  na  kwamba, anawabagua  wao  kwa  sababu  ni  watoto  wa  mama  wa  kambo.

Hivyo  basi Bundala, Kalunde  pamoja  na  mama  yao alieitwa   Bi. Mkamiti  wakaamua  kusafiri  hadi  wilaya  ya  Kasulu  mkoani  Kigoma  kwa  ajili  ya  kwenda  kumroga  Lugwisha  ili afilisike  kabisa, awe  kama  wao  au  awe  chini  yao.

------------------------------------------------------------------

JE   BEKA     MSANGI   ATAFANIKIWA   KUMUHAMISHA  LUGWISHA  KWA  KUTUMIA  UCHAWI ? JE  BUNDALA, KALUNDE  NA  BI MKAMITI   WATAFANIKIWA  KUMFILISI  LUGWISHA  KWA  KUTUMIA  UCHAWI  KUTOKA  KIGOMA ?

Jiandae  kusoma  kitabu  “  KITANDA  CHA  SOKWE  MTU “  upate  kujua  ukweli   kuhusu  kisa  hiki  cha  ukweli.   Kitabu  hicho  kitatoka  hivi  karibuni  na  utakipata  kwa  gharama  ya  SHILINGI  ELFU  KUMI  TU  ZA  KITANZANIA .

Katika  kitabu  hicho  utapata  kufahamu  mambo  mbalimbali  kama  vile ;

A. Jinsi  wachawi  wanavyo  tengeneza  uchawi  wa  kumuhamisha  na  kumfukuza  mtu   kwa  kutumia  uchawi, kutoka  sehemu  moja  na  kwenda  sehemu  nyingine  na  kumfanya  mtu  huyu  asirudi  tena  katika  eneo  hilo  hadi  anaingia  kaburini, pamoja  na jinsi ya  kujiepusha  dhidi  ya  uchawi  huo.

B. Utapata  kufahamu  jinsi  wachawi  wanavyo tengeneza  uchawi  wa  kumfilisi  mtu  fedha  na  mali  zake  zote  kwa kutumia  uchawi  pamoja  na  jinsi  ya  kujikinga  dhidi  ya  uchawi  wa  namna  hiyo  hali kadhalika  jinsi  ya  kumzindua  mtu  aliye  tupiwa  uchawi  wa  aina  hiyo.

Vile  vile  katika  kitabu  hiki  utapata  kujua  matumizi  ya  kichawi  na  kiganga  kuhusu  vitu  na  mambo  mbali  mbali  kama  vile :

1.  Miti  ya  kwenye  kitanda  cha  sokwe  mtu

2. Mizizi iliyookotwa wakati kaburi linachimbwa

3. Dawa  chafu  ya  kiarabu  ambayo  inafanana  na  lami : Dawa hii  ya  kiarabu  ni  miongoni  mwa  madawa  machafu  kabisa  yatumikayo  kwa  ajili  ya  mambo  ya  shari  za  aina  mbalimbali. Utafahamu pia jinsi ya  kujikinga  na  heri  za  dawa  hiyo.

4.   Mzizi  ya  mti uitwao  Mbono  Kaburi

5.   Mizizi  ya  mti uitwao  Mtopetope

6. Mizizi  ya  mti  uitwao  Mshindwi

7.Marashi  ya  waridi

8. Sindano

9.Nyembe  zilizo  katwa  na  kwanini  huwa  zinakatwa

10.Makaburi  ya zamani  yaliyo  kwisha  kusahaulika

11. Jogoo  mweusi  au  jogoo  mwekundu  aliye wekwa  porini kwa  muda  wa  siku  saba.

12.Chungu  cheusi  kilicho  kesha  kaburini kwa  muda  wa  siku saba

13.Kaniki  nyeusi  pamoja  na  kamba  za  kaniki  nyeusi

14.Ngorani  yangu : Utapata  kujua  neno la  lugha  ya  kiha  “ NGORANI” lina maanisha  kitu  gani  katika  ulimwengu  wa  waganga  na  wachawi  na  linatumikaje, wakati  gani, kwa  sababu, gani, namna  gani  nakadhalika.

15.Mwiko  uliotumika  kupika  kwenye  msiba  mkubwa

16.Mzizi  wa  mti  ulio katisha  njia : Kwa  ufupi  tu  hiki  ni  kizimba  kikubwa  sana chenye  matumizi  mengi  sana  katika  ulimwengu  wa  kiganga. Ni kizima  kinacho tumika kufungua  vifungo  vingi  sana  vya  kichawi. Kila  mtu anapaswa  kufahamu  kuhusu  kizimba  hiki.

17. Maji  ya  mchele  yaliyo  kesha

18.Maji  ya  zamzam

19.Mizizi ya mti  wa  mkurungu

20.Jogoo  aliye  wika  alfajiri  mara  moja  tu na  kuchinjwa  hapo  hapo, huku damu  yake  ikiwekwa  kwenye  chungu  cheusi

21. Mizizi  ya  mti  uitwao  Mkubashengelo

22. Mizizi  ya  mti uitwao Mzungupori

23.Maseko :  Hii  ni dawa   ipatikanayo  kwa  kuchanganya  dawa  saba  za  porini ambazo, kati  ya  dawa  hizo  ni  pamoja  na  magamba  ya  mti  wa  ukwaju pori, pamoja  na  mafuta  ya  mnyama fulani  afugwae

24.  Mkuki  mdogo  wa  asili

25.Sarafu  ya  fedha

26. Asali  mbichi  ya  nyuki  wadogo

27.Panya  mdogo  aitwae  Msuswe

28. Mafuta  ya  simba

29.Mafuta  ya  nyuki  wa  Nimba : Nimba  ni  mnyama  wa  porini  ambae  anafanana  na  nyumbu. Mnyama  huyu  huwa  anatembea  na  mzinga  wa  nyuki  kichwani  kwake. Yupo  katika  kundi  la  wanyama  washirikina. Hapatikani  wala  kuonekana  kwa  urahisi na huwa  anapotea  kimiujiza.

30. Nywele  za  saluni

31. Punda, kondoo,  au  mbwa  aliye  pita  duniani  bila  kuonekana

PAMOJA   NA  MAMBO  MENGINE  MENGI.

KITABU  HIKI  KITAFUNGUA  UFAHAMU  WAKO  KUHUSU  MAMBO MENGI  KATIKA  ULIMWENGU  USIO ONEKANA.

SABABU  YA  KUTOA  KITABU : Wafuatiliaji  wa  makala  zangu  wamekuwa  wakilalamika, ninachelewa  sana  kutoa  matoleo  yanayo  fuata  ya  makala  mbalimbali  zilizo  andikwa  au  kusimuliwa  nami. Hii  imekuwa  ikisababishwa  na  kutingwa  na  shughuli  nyingi  na  hivyo kukosa  muda  wa  kutosha  wa  kuandika  makala.  Watakao  pata  bahati ya  kusoma  kitabu  hiki, watapata  fursa  ya  kukisoma  kuanzia  mwanzo  hadi  mwisho  wake.

WEKA  ODA  YAKO MAPEMA : Weka  oda  yako  mapema . Utaratibu  wa  kuweka  oda  ni  kama  ifuatavyo :  ANDIKA  UJUMBE  MFUPI  WA  MANENO  KUPITIA  SIMU  YANGU  YA  MKONONI

0744  000  473  UKISEMA  “ KITANDA  CHA  SOKWE  MTU”. Nami  nitahifadhi  namba  zako, na  kitabu kitakapo  toka  jikoni  basi utakuwa  miongoni  mwa  watu  wa  kwanza  kupata  nakala  yako.

Au  unaweza  kuandika  ujumbe  mfupi  wa  maneno  ukiambatanisha  na  namba  zako  simu  kupitia  barua  pepe  yengu : mungwakabili@gmail.com.

Kwa  maelezo  zaidi  kuhusu kitabu  hiki  na  mambo mengine  kuhusu  ulimwengu  usio onekana. Nitembelea  :  www.mungwakabili.blogspot.com