Zainabu Rajabu
MSHAMBULIAJI wa Simba Laudit Mavugo amesema kuzomewa kwake kipindi wakati hafanyi vizuri uwanjani ndiyo kumemfanya awe vizuri kwa sasa.
Mavugo alikuwa anazomewa sana na mashabiki wa Simba huku wakimtolea maneno ya kejeli pindi alivyokuwa hafungi magoli na wala hakuwa na msaada kwa timu.
Shaffidauda.co.tz ilipiga stori na straika huyo ambae kwasasa amekuwa lulu kwa wana Simba na amesema hizo zilikuwa changamoto kwake kutokana na kila shabiki kuwa na uchu wa kumuona anafunga magoli.
“Unajua mimi kama mchezaji nisipofanya vizuri mashabiki wana haki ya kupiga kelele kwa sababu wanaona mimi sina faida kwenye timu yao na ikiwa nimesajiliwa kwa pesa nyingi,” alisema Mavugo.
Raia huyo wa Burundi amesema, mfumo wa kocha wake Joseph Omog awali ulikuwa unampa wakati mgumu sana lakini kwa sasa nimeweza kuendana nao ndiyo maana napachika mabao.
Mavugo amepachika magoli saba hadi sasa kwenye ligi kuu tangu alivyojiunga na wekundu wa Simba msimu huu akitokea Vital’O ya Burundi.