SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 16 Desemba 2016

T media news

Virusi vya Zika vyagunduliwa nchini Tanzania

Image copyrightAPImage captionVirusi vya Zika vinaaminika kusababisha watoto kuzaliwa an vichwa vidogo

Taasisi ya utafiti wa magonjwa ya binadamu, NIMR imethibitisha kugunduliwa kwa virusi vya Zika nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Dkt Mwele Malecela, virusi hivyo vimepatikana mkoani Morogoro, Mashariki mwa Tanzania na Mkoani Geita, kaskazini magharibi mwa Tanzania.

Utafiti huo ulifanyika kutokana na uhalisia kuwa kuna mazingira yanayowezesha kuzaliana kwa mbu wanaoeneza virusi hivyo.

Kati ya watu 533 waliopimwa wakati wa utafiti huo, asilimia 15.6 waligunduliwa kuwa na virusi vya Zika.

Njia 10 za kujikinga dhidi ya virusi vya ZikaVirusi hatari vya Zika vyafika Afrika

Dkt Mwele Malecela ameambia BBC kwamba kwa sasa serikali inaangazia kuzuia wajawazito wasiumwe na mbu ambao wanaaminika kueneza virusi hivyo.

"Bado tunajaribu kuangalia ni aina gani ya virusi vya Zika. Lakini hiyo ni dhahiri, tukizingatia kwamba mbu wanaoambukiza Zika wako nchini kwetu na mazingira yaliyoko nchini kwetu hayatofautiani sana na yale ya Amerika ya Kusini na nchi kama Thailand ambako ugonjwa huo unapatikana," amesema Bi Malecela.

"Ugunduzi huu tumeupata kwa watu na tutaendelea kufanya kazi kuangalia kama tutaupata kwa mbu ambao utatuhakikishia basi kwamba ugonjwa huo ina maana umekuwepo nchini ni vile tu ulikuwa haujaonekana."

"Heri nusu shari kuliko shari kamili, kulielewa jambo na kujua kwamba lipo nchini na kujua kwamba wajawazito wanaweza kuzaa watoto wenye matatizo haya kutatuwezesha kuzuia ugonjwa huyu. Tutahakikisha nguvu zetu za kupambana na mbu wanaoeneza virusi hivi zinaongezeka."

Virusi vya Zika zimekuwa vikisababisha watoto kuzaliwa wakiwa na ubongo uliodumaa na vichwa vidogo katika mataifa ya Amerika Kusini na sana Brazil.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily News la Tanzania, Dkt Malecela, alipokuwa akitangaza matokeo ya utafiti huo mjini Dar es Salaam alisema uchunguzi wao ulionesha kati ya watoto 80 waliozaliwa wakiwa na matatizo ya kimaumbile, asilimia 43.8 walikuwa na virusi vya Zika.

Virusi vya Zika vyagunduliwa nchini Tanzania

Mapema mwaka huu, serikali ya Tanzania iliwaagiza madaktari wote kuwa macho kuhusu hatari ya virusi hivyo mlipuko ulipotokea nchini Brazil.

Virusi vya Zika huenezwa sana na mbu ingawa kumeripotiwa pia visa vya watu kuambukizwa virusi hivyo kupitia kufanya mapenzi.

"Msishike mimba sasa", mataifa yashauri wanawake

Haijabainika iwapo aina ya virusi vya Zika vilivyopatikana Tanzania ni vile ambavyo vimekuwa vikisababisha watoto kuzaliwa na vichwa vidogo Amerika Kusini.

Virusi vya aina hiyo viligunduliwa kwa mara ya kwanza barani Afrika katika visiwa vya Cape Verde mwezi Mei mwaka huu.

Image captionMsitu wa Zika nchini Uganda

Jina la virusi hivyo linatokana na msitu wa Zika, Uganda ambapo virusi hivyo vilitambuliwa kwa mara ya kwanza 1947.

Wengi wa walioambukizwa aina ya awali ya virusi walikuwa wakipatwa na homa ambayo si kali sana, mwasho na maumivu katika maungio.

Lakini kwa aina ya sasa, ambayo mlipuko wake ulianza mwishoni mwa mwaka 2015 nchini Brazil, dalili zake zimekuwa kali na virusi hivyo vinaaminika kusababisha kudumaa kwa ubongo na kasoro nyingine mwilini.

Historia ya kuenea kwa virusi vya Zika

1947: Wanasayansi wanaotafiti kuhusu homa ya manjano msitu wa Zika, Uganda wagundua virusi hivyo kwenye tumbili.1948: Virusi hivyo vyapatikana kutoka kwenye mbu aina ya Aedes africanus msitu wa Zika1952: Visa vya kwanza vya binadamu kuambukizwa virusi vya Zika vyaripotiwa Uganda na Tanzania1960-80: Virusi vya Zika vyapatikana kwenye mbu na tumbili maeneo ya kati Afrika1960-80: Virusi vya Zika vyapatikana maeneo yenye misitu na mvua nyingi Asia, ikiwemo India, Indonesia, Malaysia na Pakistan2007: Virusi vya Zika vyaenea nje ya Afrika na Asia, kwanza katika visiwa vya Yap kwenye bahari ya pasifiki2012: Watafiti wagundua aina mbili tofauti za virusi vya Zika, virusi vyenye asili Afrika na vingine vyenye asili AsiaMachi 2, 2015: Brazil yaripoti visa vya watu kuugua kutokana na maambukizi ya virusi vya ZikaJulai 17: Brazil yaripoti visa vya watoto kuzaliwa na ubongo uliodumaa na vichwa vidogoOkt. 30: Visa vya watoto kuzaliwa an vichwa vidogo Brazil vyaongezekaNovemba 2015-Januari 2016: Visa vya Zika vyaripotiwa Suriname, Panama, El Salvador,Mexico, Guatemala, Paraguay, Venezuela, French Guiana, Martinique, Puerto Rico,Guyana, Ecuador, Barbados, Bolivia, Jamhuri ya Dominika, Nicaragua, Curacao,Na JamaicaFeb. 2, 2016: Kisa cha kwanza cha Zika kuenezwa Marekani charipotiwa, kikidaiwa kutokana sana na ngono badala ya kuumbwa na mbu.Mei 20: WHO yatangaza kupatikana kwa virusi vya Zika kwa mara ya kwanza Afrika kipindi cha sasa cha mlipuko, katika visiwa vya Cape Verde. Virusi hivyo ni vya aina sawa na virusi vilivyosababisha watoto kuzaliwa na vichwa vidogo Brazil.Agosti 3, 2016: Wataalamu Marekani watangaza kuanza kwa majaribio ya chanjo dhidi ya Zika.