SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Jumapili, 20 Novemba 2016

T media news

Rais Magufuli amjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga aliyelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John PombeMagufuli, jana tarehe 19 Novemba, 2016 amemtembelea na kumjulia hali Mkuu wa Mkoa wa Tanga Bw. Martin Shigella ambaye amelazwa katika wodi ya Sewahaji iliyopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam.

Bw. Martin Shigella alifikishwa hospitalini hapo tangu Jumatano iliyopita kwa ajili ya kupata matibabu.

Akimpa pole wodini humo Rais Magufuli alisema “Nakupa pole sana Ndg. Martin Shigella kwa maradhi yaliyokupata, nakuombea kwa Mwenyezi Mungu upone haraka na urejee katika kituo chako cha kazi ili uendelee na majukumu ya ujenzi wa Taifa”

Hali ya Bw. Martin Shigella inaendelea vizuri.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dar es Salaam