Meli hiyo kubwa ya aina yake ya *Jeshi la Maji la China* itawasili Bandari ya Dar es Salaam ikiwa na *Madaktari Bingwa na Wataalamu wa Afya zaidi ya 380* ina uwezo wa kufanya *upasuaji mkubwa na mdogo* ndani ya meli kwa zaidi ya *Watu 600 kwa siku.*
*RC MAKONDA* amewatangazia wananchi *kuchangamkia fursa* hiyo ya huduma ya matibabu bila malipo kuanzia *November 20 -25 ndani ya Meli.*
*MAKONDA* amesema Meli hiyo itatoa matibabu kwa *Magonjwa ya Figo, Saratani, Ini, Moyo, Macho, Sukari, Presha* ambapo watakaopimwa na kugundulika kuwa na tatizo *watapatiwa Dawa na matibabu Bure.*
Aidha *MAKONDA* amesema huduma hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa *kuokoa gharama za matibabu kwa Wananchi* ikiwemo ile ya *kusafirisha wagonjwa nje ya nchi* kwakuwa ndani ya meli zitapatikana huduma zote ambazo hazipatikani kwenye hospital za Tanzania.
Hatua hiyo ni *utekelezaji wa ahadi iliyotolewa na aliekuwa Balozi wa China Nchini Tanzania* aliyoitoa wakati wa *Zoezi la upimaji wa Afya bure* ambapo aliahidi kumuunga mkono *RC MAKONDA* katika kuboresha Sekta ya Afya.
Jambo jingine litakalifanywa na wataalamu hao ni *kukarabati vifaa vyote vya hospital za Dar es salaam*vitakavyokuwa na matatizo ikiwemo Ultrasound na Xray ili ziweze kufanyakazi upya ambapo pia *madaktari hao watakuwa wakibadilishana uzoefu na utaalamu na madaktari wa Tanzania.*
Mbali na hilo Madaktari hao watatembelea *vituo vya kulelea watoto yatima* kujionea namna serikali inahudumia watu Hawa wa kundi maalumu pamoja na siku ya moja ya *kubadilishana utamaduni wa mavazi, vyakula na michezo*.
*RC MAKONDA* amemwambia Mganga Mkuu wa Mkoa *kuwaita Wagonjwa wote waliokuwa wamepangiwa kufanyiwa upasuaji tarehe za mbali kutokana na ufinyu wa huduma kupelekwa kufanyiwa huduma Bure.*
Nae Kamanda wa Jeshi la Maji la China *Meja Xing Song* amesema zoezi hilo ni matunda ya ushiririkiano wa kidiplomasia baina ya Tanzania na China ambapo wamesema watazidi kushirikiana na *RC MAKONDA*