SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Ijumaa, 23 Februari 2018

T media news

Nyani Aiba Mamilioni Katika Nyumba ya Kiongozi wa Siasa

Ikiwa ni wiki chache tu zimepita tangu kutokea kwa tukio la aina yake la nyoka kumeza mamilioni ya fedha nchini Nigeria, hali hiyo ya kustajabisha imeendelea kujitokeza ambapo kwa sasa nyani anadaiwa kuiba fedha kiasi cha Naira milioni 70 (sawa na shilingi za kitanzania milioni 436), kutoka katika nyumba ya Seneta iliyoko eneo la mashambani.

Soma hapa nyoka atafuna mamilioni na kutoweka

Tukio hilo la aina yake na la kushangaza limetajwa kutokea katika nyumba ya Seneta Abdullahi Adamu aliyekuwa mwenyekiti wa Jukwaa la Maseneta wa kaskazini nchini humo, ambapo fedha zilizokuwa zimekusanywa katika awamu ya 7 wa seneti, zilitakiwa kukabidhiwa kwa mwenyekiti wa awamu ya 8 ya seneti hiyo.

Nyumba hiyo inayotajwa kuwa katika eneo la mashambani ambapo kuna wanyama mbali mbali ikiwemo nyani.

Kufuatia kutokea kwa tukio hilo, jukwaa la Seneti limemvua madaraka ya uenyekit, aliyekuwa mwenyekiti wake Seneta Abdullahi Adam, kutokana na uzembe huo huku hatua zaidi za kisheria zikifuatwa.