SASA UNAWEZA DOWNLOAD T MEDIA NEWS APPS.

Alhamisi, 4 Mei 2017

T media news

Mimi ni shabiki wa ‘kutupwa’ wa Arsenal’ – Pro. Lipumba

Mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF) taifa Mh. Prof. Ibrahim amesema yeye ni shabiki wa kutupwa wa Arsenal licha ya klabu hiyo ya England kutotwaa mataji makubwa kwa muda mrefu.

“Arsenal haifanyi vizuri, lakini ndio timu yangu ninayoipenda,” Prof. Lipumba amesema kwenye kipindi cha Clouds 360 cha Clouds TV leo Alhamisi Mei 4, 2017 wakati akitoa ufafanuzi wa mambo mbalimbali yanayohusiana na chama chao (CUF).

Lipumba pia amesema yeye amewahi kucheza soka wakati akiwa mwanafunzi wa shule ya sekondari japo haikua kwa kiwango cha ushindani.

“Nimewahi kucheza mpira wakati nasoma sekondari, lakini sio katika ngazi ya ushindani,” amesema Pro. Lipumba.