Mama Madogo wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dkt Jakaya Kikwete, Nuru Khalfan Kikwete amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mbunge wa Chalinze na Mjukuu wa Bibi huyo, Ridhiwani Kikwete amethibitisha taarifa za kifo hicho ambapo ameandika kupitia ukurasa wake wa Instagram “TANZIA Ndugu na Marafikia nasikitika kuwatangazia Msiba/Kifo cha Bibi Yetu Bi.Nuru Khalfan Kikwete Kilichotokea asubuhi hii katika Hospitali ya Muhimbili alipokuwa amelazwa kwa Matibabu. Taratibu za mazishi tutajulishana . Innallilllah wainnaillah rajuun.”