Zainabu Rajabu
STRAIKA wa Yanga Obrey Chirwa amesema bado wana nafasi ya kuchukua ubingwa wa ligi kuu Tanzania bara ikiwa bado wataendelea kupambana vizuri kwenye mechi zijazo ili kupata matokeo mazuri.
Chirwa ambae kwasasa amekuwa na msaada mkubwa katika kikosi cha Kocha mkuu George Lwandamina, huku akiwa amepachika magoli nane katika ligi kuu tangu alipo sajiliwa na Yanga akitokea Platinum ya Zimbabwe.
Chirwa ameiambia shaffihdauda.co.tz: “Huwezi kututoa kwenye mbio za ubingwa kwa mechi mbili ambazo kwetu tumeambulia alama moja.
“Mimi bado naamini tukishikamana vizuri kuanzia viongozi hadi wachezaji nina imani kombe linabaki mitaa ya Jagwani,” alisema Chirwa.
Nyota huyo ambae usajili wake ulizua gumzo kwa mashabiki hadi kwa wazee wa Yanga kama (mzee Akilimali) huku wakimuona hafai amesema penati aliyokosa Msuva ilisababishwa na uwanja kuwa mbovu.